Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, 9 February 2019

Rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa amaliza muda wake wa usuluhishi wa mgogoro Burundi

Benjamin Mkapa
Rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa amemaliza kipindi chake cha usuluhishi wa mgogoro wa kisiasa nchini Burundi na wala hajajiuzulu, ofisi yake imesema.

Awali taarifa zilizagaa kuwa Mkapa amejiuzulu majukumu hayo kwa kupewa ushirikiano finyu kutoka kwa uongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambao ndio ulimpa Mkapa jukumu la usuluhishi.
Mzozo wa kisiasa nchini Burundi ulianza mwaka 2015 baada ya rais President Pierre Nkurunziza kugombea na kushinda urais kwa awamu ya tatu.

"Muda wake wa usulihishi umefikia tamati, hajajiuzulu," msemaji wa Mkapa, Makocha Tembele ameiambia BBC Idhaa ya Kirundi.

Tembele ameiambia BBC kuwa rais Mkapa amewasilisha ripoti yake ya mwisho juu ya usuluhishi wa mgogoro huo kwenye mkutano wa Viongozi wa Nchi wananchama wa EAC mapema mwezi huu jijini Arusha.

Kwa mujibu wa msemaji huo sasa kazi inabaki kwa rais wa Uganda Yoweri Museveni kuendelea na sehemu inayofuata ya usuluhishi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot